Friday, August 29, 2014

SHEIKH MWAHUTA ALEZEA MAZITO MSIKITI WA MSHINDO

Mwalimu wa Markazi ya
wamisri nchini Tanzania
tawi la Iringa, Kitanzini
Islamic Centre Sheikh
Salum Mwahuta jana
ijumaa alikhutubia
waislamu katika Msikiti wa
mshindo huko Iringa, na
kuzungumza mambo
mazito ambayo
mwanadamu aliyoneshwa
na Allah kabla ya kuja
kwake Duniani.

Sheikh Mwahuta katika
khutuba yake hiyo pamoja
na mambo mengine
alielezea pia namna ya
binadamu alivyoumbwa na
muda uliyopita kabla ya
kuletwa kwake hapa
duniani.

Sheikh Mwahuta kitalamu
ni mfasiri wa Qur-an
ambaye pia ni mtaalamu
wa somo la mirathi ya
kiislamu, mwahuta
alihitimu masomo yake
miaka kadhaa iliyopita
katika chuo kikuu cha
Azhar na kujipatia fani
mbali mbali kutoka kwa
marehemu Sheikh Twantwi
aliyekuwa sheikh Azhar
kipindi hicho.

Sheikh Mwahuta hutoa
khutuba za ijumaa katika
misikiti mbali mbali
mkoani Iringa ambapo ndo
makaazi yake yalipo kwa
sasa katika maeneo ya
Iringa Mjini Mtaa wa
Mwangota.

Khutuba ya Sheikh
Mwahuta inapatikana kwa
njia ya whatsapp tuma
inbox neno khutuba
ambatanisha na namba
yako ya whatsapp
utatumiwa kabla
haijawekwa online.

chini picha ya Sheikh
Mwahuta akiwa amemshika
mkono Sheikh Mohammed
Twantwi aliyekuwa Sheikh
wa Azhar kipindi hicho.

Thursday, August 28, 2014

TSC FC KUENDELEA NA MAZOEZI HAPO KESHO

Tanzania Stars in Cairo (TSC FC) kesho wanatarajia kushuka uwanjani kuendelea na mazoezi yao ya kila wiki katika uwanja wa Citadel maeneo ya Saida Aisha.

Akizungumza na ripota wetu kocha na mdhamini wa timu hiyo ndugu Abdallah Matitu (baba fahdy) alisema kuwa
Mazoezi yataanza saa 4:00pm mpaka 5:00pm, na kuomba wachezaji kufika mapema ili kwenda sambamba na ratiba ya mazoezi.
pichani kocha na mdhamini wa timu hiyo (wakwanza kushoto) akiwa na mchezaji tegemeo Twaha kizuki (Galabwana) alipotembelewa na kocha huyo maeneo ya bouth Hostel ili kuzungumzia mkataba wa mchezaji huyo ambao unaisha hivi karibuni.

Monday, May 5, 2014

SHEIKH ILUNGA HASSAN KUZIKWA LEO DAR

Sheikh ilunga Hassan Kapungu alifariki dunia jana usiku baada ya kuugua kwa muda mrefu akisumbuliwa na maradhi ya sukari na baadae figo kushindwa kufanya kazi.

Sheikh Ilunga amefariki katika jiji la Dar es Salaam, anatarajiwa kuzikwa leo katika Makaburi ya Mwinyimkuu yaliyoko Magomeni Mapipa.

Maiti yake itasaliwa katika msikiti wa kichangani magomeni Dar es Salaam katika sala ya Alasiri saa kumi jioni.

Sheikh Ilunga ambaye alikwenda nchini India kwa matibabu aliwahi kukamatwa na polisi na kufunguliwa mashtaka kwa tuhuma za kutoa mahubiri ya uchochezi, msiba wake upo Mbezi Goigi.

Mwenyezi Mungu amsamehe makosa yake na amuingize katika pepo ya juu,aamin.

SHEIKH ILUNGA AFARIKI DUNIA

Taarifa  zilizotufikia kutoka kwa watu wetu wa karibu zinasema kwamba Muhubiri wa Kiislamu nchini Tanzania na Afrika Mashariki dunia Sheikh Ilunga amefariki Dunia kwa ugonjwa sukari.

Wednesday, May 22, 2013

Gari ya Kwanza Inayopaa Juu

Shirika la Valkswagen linalojihusisha na utengenezaji magari, mara hii limekuja kivyengine kwa kutoa gari inayopaa juu kama ndege, gari hiyo yenye uwezo wa kubeba watu wawili, itakua inatumia barabara za kawaida ila hii itakua inaruka juu.
Gari hii mpya haina matairi kama ya gari la kawaida inauwezo wa kupaa bila ya kukimbizwa kw vile inavyokua ndege, katika pita pita yake barabara inasubiri mataa kama gari la kawaida.

Saturday, May 18, 2013

Markazi, Tanzania Students' Center in Cairo, (TSCC).


Markazi, Tanzania Students' Center in Cairo, (TSCC).

Imeanza kuaanda Film za simulizi za kweli (documentary),
hii ni hatua mpya kwa kituo hichi cha Markazi kuanaanda  film za aina hiyo.
Filim hizo zitaanza kurusha baada ya mitihani kupitia Channel yetu ya Youtube ijulikanoyo kwa jina la Markazi Cairo.
Markazi inawalika wale wote wataopenda kuandaliwa film za simulizi za kweli wafike katika ofisi zetu zilizopo Maida Geishi,Jumba No. 6 Ghorofa ya 5.

Tuesday, April 16, 2013

Bungeni hakukaliki, kauli za kejeli na kuudhi zatawala


Dodoma.Baadhi ya wabunge jana waliendelea kutumia fursa ya mjadala wa hotuba ya Waziri Mkuu kurushiana vijembe na maneno ya kuudhi mambo ambayo yalisababisha mivutano ya kikanuni, huku mmoja wao akionya kwamba ikiwa haki hiyo itaendelea bungeni hakutakalika.

Chimbuko la mivutano hiyo ni kauli zilizotolewa na Mbunge wa Kondoa Kusini (CCM), Juma Nkamia ambaye alimjibu Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi kwamba “haongei na mbwa bali anazungumza na mwenye mbwa.”

Kadhalika Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde aliwapiga vijembe viongozi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akisema kwamba kuna wabunge ambao wana “mimba zisizotarajiwa bungeni”.

Vijembe hivyo viliendelea jioni baada ya Mbunge wa Nyamagana (Chadema), Ezekiah Wenje kusema Serikali iliyopo madarakani haina uwezo, haina ujuzi na imepoteza imani ya watu kutokana na kushindwa kuwatatulia wananchi matatizo yaliyopo.
Naye Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa akieleza kuwa Serikali ina tatizo kwa kuwa kuna “akili ndogo inatawala vichwa vikubwa.”

Alitumia kifungu cha kitabu kitakatifu cha Biblia cha Mithali 27:22 kinachosema kuwa “mpumbavu ukimchukua ukimchanganya na ngano kwenye kinu atabaki na upumbavu wake.”
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisema Wenje na Msigwa walikiuka kanuni za Bunge kutokana na matamshi yao.

Sunday, January 13, 2013

Afrika ya kati ; makubaliano yatiwa saini


Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Francois Bozize amemfuta kazi waziri wake mkuu na kulivunja baraza lake la mawaziri Jumamosi(12.01.2013)akisafisha njia kwa kuteuliwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa.
Serikali  na  waasi  wa  muungano  wa  Seleka , ambao  walisonga mbele  katika  mashambulizi  yao  hadi  karibu  na  mji  mkuu  Bangui mwezi  uliopita, wamekubaliana  kuunda  serikali  ya  mpito mwishoni mwa   mazungumzo  yao  yaliyofanyika  katika  mji  mkuu  wa  Gabon , Libraville  siku  ya  Ijumaa(11.01.2013).
"Kiongozi  wa  nchi, ameondoa matumizi  ya  amri  iliyotolewa  Aprili  22, 2011, inayohusiana  na  kuteuliwa  kwa  serikali," imesema  amri  ya  rais iliyosomwa  katika  televisheni  ya  taifa. Soma Zai didw.de

Saturday, January 12, 2013

Tanzania Students' Center in Cairo

Baadhi ya wanafunzi wa Markazi ya watanzania Misri (TSCC) kutoka mataifa mbambali wakimsikiliza mwalimu wao (hayupo pichani) kwa umakini na uangalifu kwenye somo la Kingereza. Markazi inafundiasha lugha mbalimbali ikiwemo Kiswahili,Kingereza,Kiarabu na Kichina,kama ambavyo kituo hakikujiweka nyuma kwani kinafundisha Masomo ya Computer na ufundi wake.

Wednesday, January 9, 2013

Mapigano ya kikabila yazuka tena Kenya

Kulingana na Caleb Kilunde afisa wa shirika la msalaba mwekundu, watu wawili kati ya wanane waliouwawa wanaaminika kutoka katika kundi la washambuliaji walioanza kuishambulia jamii ya wa Orma katika kijiji cha nduru. Caleb amesema watu wengine watatu walipata majeraha mabaya ya kichwa na kwamba hali mpaka sasa ni ya wasiwasi kwa kuwa harakati za kulipiza kisasi huenda zikawa zinapangwa.
Kulingana na Caleb Kilunde afisa wa shirika la msalaba mwekundu, watu wawili kati ya wanane waliouwawa wanaaminika kutoka katika kundi la washambuliaji walioanza kuishambulia jamii ya wa Orma katika kijiji cha nduru. Caleb amesema watu wengine watatu walipata majeraha mabaya ya kichwa na kwamba hali mpaka sasa ni ya wasiwasi kwa kuwa harakati za kulipiza kisasi huenda zikawa zinapangwa. Soma Zaidi DW

Mzozo wa gesi washika kasi Tanzania

Rais JK

Mzozo wa gesi ya Mtwara kusafirishwa jijini Dar es Salaam unazidi kufukuta, ambapo sasa madai hayo yanapata uungwaji mkono kutoka katika makundi mbalimbali ya watu wakiwemo viongozi wa dini na wasomi.
Huku mzozo wa gesi ya mkoa wa Mtwara kusafirishwa jijini Dar es Salaam Tanzania ukizidi kufukuta, sasa baadhi ya wachambuzi nchini humo wanaungana na wakaazi hao wakisema kuwa wana madai ya msingi ya kutaka mkoa wa Mtwara moja kati ya mikoa maskini nchini humo kufaidika na mapato ya gesi hiyo kabla ya taifa zima kunufaika na rasilimali hiyo. Soma zaidi DW

Friday, January 4, 2013

Alichokisema Aliyekua katibu wa Chadema Mbeya, Edo Makata baada ya kujiuzulu CHADEMA

Aliyekua katibu wa Chadema Mbeya, Edo Makata


Ndugu waandishi,
Niruhusu niorodhesha sababu zinazoniondoa CHADEMA kuamua kuwa huru hadi hapo nitakapotangaza ama kuendelea na siasa au nabaki kuwa mtumishi wa taasisi ninakofanyia kazi na ujasiliamali wangu.
1. Bado sikubaliani na Ndugu Slaa kuwa na kadi ya CCM. Nataka airudishe ama awajibike kisiasa.
2. matumizi ya Ruzuku si sahihi. Mikoa, Wilaya, kata hawapewi pesa zaidi ya wao kujichangisha. Huku Maafisa wa makao Makuu wakiishi kama wafalme na Malkia.
3. Mgawanyo wa rasilimali za chama ni utata mtupu, Mkoa kama Mbeya, wenye CHADEMA ya kweli kwa sasa haujapewa hata kipaza sauti wakati magari yote na vifaa vyote vimehodhiwa na Makao Mkuu, hii ni zaidi ya ufisadi tunaopiga kelele. Kuwafanya wanachama wa Mikoani ni kuku wa kienyeji kwa kuwarushia punje za mchele unapotaka kuwachinja. Mikoani viongozi na wanachama wanatoa pesa zao kwa kujichangisha kwa imani kuwa siku moja watakula keki ya Ruzuku na ufadhili. Mimi nawahakikishia , kwa unyenyekevu nilioufanya hawatopata hadi Mbowe na Slaa watoke kwenye nafasi walizo nazo kwa sasa. Wasidanganywe na siasa za mikutano ya matumaini ya kitaifa yenye posho.
3. Mfumo wa Demokrasia ndani ya chama haufanani na kelele tunazozipiga kwa wananchi wengi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu (3K), Kimsingi CHADEMA tunauhaba wa Demokrasia. Mfano:
(i) Mchakato wa mgombea uraisi (2010) ndugu Slaa kamati kuu ilipendekeza jina lake na kuitisha Baraza kuu na mkutano mkuu Tukavumilia.
(ii) Wagombea ubunge nikiwemo mimi tulitumana tu kwenye majimbo kwa lengo la kuibana CCM- tumevumilia. Viti maalum, tumevumilia. Sasa hivi ukitaka kugombea jimbo unatakiwa kuandika barua makao Makuu;, huu ni utawala wa ki-ubwenyenye ndani ya chama kuwafanya wapinzani wako wakudhuru au wakuzidi kete kwa mbinu za kujuana makao Makuu.
(iii) Kitendo cha mwenyekiti wa chama Mhe,Freeman Aikael Mbowe (Mb) kiongozi wa kambi Rasmi ya upinzani kuropoka, eti Ndugu Slaa atakuwa ndiye ngombea uraisi mwaka 2015 ni cha kuua kabisa Demokrasia ndani ya CHADEMA. Tena ninamshauri bure kakangu ninayemheshimu kwa siasa zake; atubu kama aliwahi kumshambulia Yusuf Makamba alipokuwa katibu mkuu – CCM aliposhikilia bango, kuwa mgombea mwenye mtaji ni Jakaya Kikwete. Mbowe awaombe radhi wanachama na wananchi wapenda mabadiliko. Hawezi kuwaburuza wasomi kama prof. Baregu, Prof. Safari, Dk. Kitila Mkumbo na wengine wengi. Leo hii mimi ungeniuliza nani anafaa kuiendesha CHADEMA ngazi ya Taifa ningesema Dk. Kitila ni wakati wake wa kuacha kazi Serikalini na kuwa katiba mkuu wa CHADEMA. Hata kuingizwa kwenye mchakato wa ugombea nafasi za juu za nchi.
4. Migogoro isiyo na suluhu wa mlingano katika kuitatua. Mfano ni Mwanza na Arusha. CHADEMA imefukuza Madiwani, lakini Karatu nyumbani kwa Slaa wanabembelezwa, hapa pana ajenda ya kuifanya CHADEMA iwe ni SACCOS tu ya wajanja wachache. Kuna kundi linatafuna fedha za chama.
5. Maandamano ya kudai haki: Hata siku moja hayajaitishwa Moshi, Karatu ili nako wananchi wa kule waonje joto ya jiwe kupambana na polisi, Maandamano ni Mbeya, Mwanza, Arusha ambako viongozi wao wanafukuzwa wakiongea ukweli au kutoa hoja zenye mantiki.
6. Matumizi yasiyo sahihi ambapo Viongozi huomba mchango kwa wanachama halafu hutumia kadri wanavyoona inafaa jambo ambalo ni fedheha kubwa na wananchi ni lazima watambue haya.
Pia upandikizaji wa siasa za uchochezi katika Vyuo Vikuu ni hali iliyosababisha baadhi ya wanafunzi kufukuzwa na chama kutowasaidia kutatua migogoro yao na serikali, Uongozi wa Vyuo.
Ndugu waandishi,
Kuna hoja tunaendelea kuzilea ndani ya CHADEMA na hatimaye zimezaa ulemavu wa Demokrasia ya kibabe Mfano: Suala la Ukanda kuwa na nguvu Kaskazini lina nafasi yake. Hoja inafuatia manyanyaso ayapatayo Zitto Kabwe (Kigoma), Arfi Said (Rukwa), Shibuda (Maswa) Juliana Shonza (Mbeya), Naombi Kaihula (Mbeya), Nyimbo (Iringa).
Ndugu waandishi,
Dhambi hii ya dhana ya ubaguzi inajikita kwenye ubaguzi wa dini na ukabila. Leo hii Zitto na Arfi ni waislamu, CHADEMA haiwataki, na hao ndiyo nguzo ya Waislamu ndani ya CHADEMA haiwataki, na hao ndiyo nguzo ya Waislam ndani ya CHADEMA, ukiwaondoa tunabaki Wakristo tupu. Halafu unasema chama kiongoze ‘DOLA’ huu ni utani wa utawala kwa Taifa kama Tanzania.
Ndugu waandishi,
Kurugenzi zote nyeti Makao Makuu yaani za fedha, utawala, habari zimekamatwa na watu wa Kaskazini. Bado kelele za marehemu chacha waugue hazirekebishi pia kitabu alichoandika ndugu Deo hakiwafundishi lolote. Chama kimeendelea kuwa NGO.
Uwezo wa Slaa kuwa Mtawala ni mdogo, hupendelea kusikiliza majungu na huvutiwa na wanaomsifia tu. Watu kama mimi tunaojenga hoja hatupandwi na tunageuka maadui kwake na wapambe wao nawasihi waache ubabe, chama ni mali ya watanzania si chao pekee.
Hapa pana mchezo wa Pwagu na Pwaguzi mmoja kusema nina kadi ya CCM na mwingine kutangaza mgombea uraisi. Hawa viongozi wanaelewa wanachokisema, hawakosei. Chukulia usemi huo wa kukiri kuwa na kadi ya CCM ungewtamkwa labda na Zitto Kabwe au Shibuda. Kamati kuu ingetishwa na haraka wangefukuzwa dalili za kauli hizi ni ishara kwa Zitto Kabwe kuwa mawazo yake ya kulitumikia Taifa ndani ya CHADEMA yanasafari ndefu. Hatokaa salama kisiasa. Hao wakubwa wameamua kuua chama ama kujibinafsisha, maamuzi magumu ni kuwatoa wao, CHADEMA itayumba baadaye itasimama.
Ieleweke kuwa kupendwa kwa CHADEMA ni kwa sababu ya Watanzania wana haja ya kuona chama kingine kinatawala. Nani alimjua Slaa ndani ya CHADEMA tangu 1995 hadi 2007 kabla ya Zitto kutolewa nje ya vikao vya Bunge? Hoja ya Mafisadi aliyopewa – Mwembe Yanga ndiyo aliyomnyanyua hadi leo. Lakini je, yeye anamiliki mali zinazofanana na Utumishi wake kama Padri na baadaye Mbunge? Ajibu! Kwa nini hoja ya Ufisadi kaizima? Muulizeni mali zake ndani ya nchi na nje wanakoishi watoto wake (Uingereza).
Leo watu wa Mbeya tunaambiwa tumzomee Rais Kikwete tuchome barabara na kuharibu uchumi. Raisi wa nchi anaona Mbeya kama kisiwa, lakini Slaa anamwita Kikwetge CCBRT anamsifia sana, Mbowe anafanya kazi na Raisi kule Hai – Kilimanjaro anamsifia sana. Mbunge wa Mbeya Mjini anapayuka Bungeni Mbeya wanamkataa Raisi. Lazima watu wa Mbeya tushituke, tumwache Raisi afanye kazi ya kuleta Maendeleo maana ndiye aliyeapishwa ndiye aliyeshinda uchaguzi – akatangazwa.
Wote waliomkataa ndani ya Bunge wanashinda na safari za Ikulu kunywa naye chai huku Mbeya tunaambiwa mkataeni. Hapana. Hii michezo ya siasa za kidhalimu tuishitukie. Mbeya tunapuuzwa na Jiji letu litachelewa kupata Maendeleo yanayolengwa na Miji ya Arusha na Mwanza. Tuseme Slaa na Mbowe yatosha kuwatumia watu wa Mbeya kama mtaji wa maandamano.
Ndugu waandishi,
Mimi naifahamu vizuri CHADEMA, nimekuwa mgombea Udiwani 2005 (Kata ya Mabibo –
DSM) na mgombea ubunge Jimbo la Kyela – 2010. Nimekuwa kiongozi ngazi ya Mkoa
Mbeya – Katibu wa Mkoa na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa. Pia nimeshika nafasi
kadhaa Mkoa wa Dar es salaam kabla ya kuja Mbeya. Hawa wana siasa wengi walio
ndani ya CHADEMA ni waganga njaa tu mle ndani ni wachache sana wanafikiri mageuzi
ya kiuchumi na utawala kwa taifa letu.
Hivyo nathibitisha mbele yenu kuwa hakuna mtu ndani ya upinzani na hasa CHADEMA
ama CCM atasema hajawahi kuhonga wala kuhongwa. Kama slaa ni msafi kama anavyotamka basi asimame mbele ya umma na athibitishe haya. Ndiyo maana hoja ya ufisadi haiendi kiutekelezaji wa vitendo. Mimi najua viongozi wa CHADEMA wanavyo tumia rasilimali za walipa kodi na misaada
ndugu waandishi,
Wapo watakaosema nimetumwa, nimehongwa, sitawapuuza, maana hao ndio walioeneza na kusambaza meseji nyingi wakitaarifu watu nimehongwa. Siasa za kutumika mimi sina, sijawahi kukaa kikao au kupewa pesa na CCM niishambulie CHADEMA. Ni vema viongozi wangu wangekuwa na hulka ya kuniuliza, vipi imekuwaje? Lakini wao hukimbilia kuwaambia wanachama – huyo mbaya sana, kapewa pesa, kala mwenyewe, mfukuzeni, hizi ni kauli au vitendo visivyo vya kizalendo kwa Taifa letu na kupandikiza chuki watu ili tuanze siasa za kuviziana. Nasema waliyosema ni uongo, uzandiki na unafiki wa Demokrasia.
Hivyo nikiwa ni kijana, bado nitafanya siasa na kikundi ninachoona kinafaa kwa wakati huo na sijutii kufanya maamuzi haya ila inaniuma kuona kazi niliyoifanya ya mageuzi inapuuzwa kwa tamaa ya wachache kukimbilia kujilipa mamilioni kama mishahara.
Nimalizie kwa kusema, nawataka wabunge wangu na hasa Joseph Mbilinyi na Msigwa – wafanye kazi ya kutekeleza ahadi zao na za chama. Tuliwaahidi wana Mbeya; bandari kavu, masuala ya Elimu, Maji, afya, ujasiliamali, amani, upendo, na kukuza vipaji vya wasanii. Lakini leo hii tunawajengea mfumo wa fujo.
Uongozi wa wilaya ya mbeya mjini ni wa mapinduzi kila kukicha kama utawala wasomalia: viongozi waliopo ni makanjanja wa kupindua wenzao kwa uroho wa ruzuku. Wamepewa kazi ya kufukuza watu uanachama na tayari wamewafukuza wengi na wanaendelea. Chama ni kufukuzana bila kufuata katiba na kuendesha mikutano ya matusi bila hoja za ujenzi wa umma mpana na bora. Wanawatuma wanachama wanishambulie eti nimehongwa.
Ujanja wa kuwateka watu na shida zao kupitia majukwaa uwe na huruma. Wakae chini waendeshe siasa za maendeleo na si kuwaza fujo na matusi. Wajifunze kutenganisha maendeleo yanayoletwa na serikali kuu kama barabara za jiji la Mbeya na Ubunge kama taasisi.
Ndugu waandishi,
Nawasihi wananchi wangu wa Jimbo la Kyela, wasinione msaliti, bali wanishauri namna ya kuimarisha harakati za kujiletea maendeleo Jimboni kwetu. Waelewe nimeshindwa siasa za sasa za CHADEMA ni siasa chafu na zenye upendeleo. Bado mimi ni mdau wa maendeleo Jimboni kwangu.
Wakati ukifika nitatangaza naingia chama gani na nitaendeleza harakati zangu za kuchochea maendeleo ya Taifa langu. Nitatimiza kazi ya uzalendo kwa nchi yangu. Wala sitaogopa kelele za wapuuzi wanaoeneza nimehongwa wakati najenga hoja. Waendelee kusambaza taarifa ambazo ingekuwa ni kazi ya CCM. Dhambi ya viongozi wa CHADEMA kuninyanyasa, kunitukana, kunidharau, na kuniundia tuhuma na kauli za kunichonganisha na umma, ipo siku itawarudi.
Naomba niwashukuru kwa kunisikiliza na salam kwa wanasiasa uchwara waliojaa siasa chafu na kazi yao ni maslahi binafsi.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
_________________________________________________________________
3
16.Haki ya faragha na ya usalama wa mtu.
17.Uhuru wa mtu kwenda atakako.
Haki ya Uhuru wa Mawazo
18.Uhuru wa maoni.
19.Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
20.Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine.
21.Uhuru wa kushiriki shughuli za umma.
Haki ya Kufanya Kazi
22.Haki ya kufanya kazi.
23.Haki ya kumiliki mali.
24.Haki ya kupata ujira wa haki.
Wajibu wa Jamii
25.Wajibu wa kushiriki kazini.
26.Wajibu wa kutii sheria za nchi.
27.Kulinda mali ya Umma.
28.Ulinzi wa taifa.
Masharti ya Jumla
29.Haki na wajibu muhimu.
30.Mipaka kwa haki, uhuru na hifadhi kwa haki na wajibu.
Soma zaidi

Thursday, January 3, 2013

Muonekano wa Jiji la Dar

                                                                     Jiji la Dar
                                                                 Ramani ya Tanzania

Tanzania Tours Tanzania Map


Mkuu wa kituo cha Markazi

Rais  Mstaafu wa Umoja wa Wanafunzi wa Afrika wasomao nchini Misri, ambae pia ni  Mkuu wa kituo cha Markazi  (Tanzania Students` Center in Cairo) Ndugu, Ally Mwinyihindi akielekeza jambo  kwa wanafunzi (hawapo picha) 



Happy New Year

Tanzania Students` Center in Cairo

Sunday, October 14, 2012

Please Keep Your Problem Child Away from My Kid


The same goes for kids. While I like to teach my kids about tolerance and differences, sometimes things go beyond that. Sometimes my kids get put into situations where they must interact with "problem children." And when that happens, and the other parents could care less ... that's when I get ticked off.
My two boys recently signed up for tennis lessons, along with two of their friends. It's a small group of just the four of them and one instructor. Since my kids are generally allergic to anything involving exercise, my wife and I were beyond ecstatic that they wanted to play tennis. So we signed them up in a heartbeat.
The first week was great, but at the second lesson, there was a new kid in their group. The problem is, this kid definitely has some issues. Anger management being one of them. He'd get crazy frustrated if he missed a ball (which was often), and took it out on the other kids. He'd scream and make fun of my kids, as well as throw tennis balls at them.
At a break, my wife actually talked to all five kids and said something along the lines of, "We'll all go in and be nice to each other now, right?" Everyone seemed fine, went back in and the abuse simply continued.
Like I said, this kid has problems. And that's fine. I've dealt with that oodles of times already, as have my kids. Heck, my own kids can act up too, and I'm quick to dive in and make sure they apologize and behave. But in this instance, what steamed me up to no end was the kid's mother. She just sat there watching her boy. Not saying a word to us or the instructor. Clearly she knew he had issues, so why wasn't she on him to make sure he behaved?
On the one hand, I feel somewhat bad for her and the kid. He has problems and it must be real tough dealing with them. I can't imagine that kid has many playdates. Part of me wants to reach out and say it's okay, let's work together, maybe the kids can become friends, etc.
But on the other hand, I'm paying good money for these lessons. I don't need to have both my kids verbally and even physically abused by another kid, simply because his mom just wants to sit there and do nothing.
We've already spoken to the instructors and hopefully they'll be moving him to another group. But that's not the point. I still for the life of me don't understand "sideline" parents. Ones who just sit and watch their kids wreak havoc everywhere without dealing with any consequences to their actions.
If they want sympathy or compassion for what they're going through, parents of problem children need to be much more involved with their kids in public. Otherwise, by just sitting there quietly, they're trying to give off the impression that their kid is fine and it's everyone else who has the problem. And I have a problem with that.

The Truth Behind "Enhanced" Waters



Drinking plain old water can be a bit of a snoozefest, especially if you're getting your recommended daily amount of at least eight large glasses a day. But if your ennui is leading you to load up on seemingly healthy bottled-water alternatives, you need to read this first.
"In general, we have no evidence that water can be improved," says Prevention's nutrition advisor David Katz, MD, MPH, an associate professor adjunct in public health at Yale University's School of Medicine. "There is no convincing evidence of benefit from any version of 'enhanced' water."
In general, he says, "we consider a beverage 'water' if it has no calories, no sodium (or trivial amounts in mineral water), and no sweetener (sugar, alternative, or artificial). If a product is sweetened, it's not water—it's a soda

Saturday, October 13, 2012

Surprising Tools That Slow Down Browsing

.


When you first got your computer, you practically flew around the Internet. But if loading websites now takes forever, some simple housekeeping can help you speed up your browsing. So let's roll u
p our sleeves and get going.

First, think of your browser as a bike; the more baggage you load onto it, the slower you go, so start streamlining.

Browser History
You can delete a lot of baggage if you clear your browsing history. All browsers store data from the sites you've been to. It's great if you want to remember where you've been recently on the web, but it can also slow the browser. Getting rid of that data can speed up how fast pages load.

In Internet Explorer, hit Tools, Internet Options, general tab, and then, under Browsing history, click Delete.
In Firefox, choose Tools, Clear Recent History.
In Chrome, hit the wrench icon in the toolbar, choose History and Clear All History.

Toolbars
Toolbars are notorious resource hogs. If you aren't using a toolbar multiple times each day, ditch it. In Firefox, go to Tools, Add-ons, and Disable Toolbars. Chrome doesn't have toolbars per se.

Add-ons and Extensions
These are like toolbars but may be running in the background, meaning they are less visible. It's a good idea to check to see you are really using these tools enough to merit their resource consumption.

In Internet Explorer, go to tools Internet Options, Programs tab, and Manage Add-ons. You'll see all the add-ons that are enabled. I say disable everything but the Shockwave Flash add-on.
In Firefox, hit Tools, and uninstall everything you can.
In Chrome, go to Tools, Extensions and disable everything you can

Bookmarks and Favorites
Another drag on your browser comes from bookmarks. You thought you were being so organized with a few hundred bookmarks neatly filed by topic. But they can make your browser slower too. Limit them to 20 or so, and keep the rest in a Word document on your desktop.

To Export Bookmarks
In Internet Explorer go to File, Import/Export and choose Export To A File, then choose Favorites. Open the HTML file it saves, copy everything and paste into a Word document. In Firefox you can open Bookmarks and copy the ones you want, then paste into a Word doc. In Chrome, go to bookmarks, Bookmark Manager, and Export. Open the HTML document it saves, copy all, and paste into a Word doc.

Defragmenting
Defragging your hard-drive is a well-known tool for speeding up all aspects of computing — even web browsing. Hit Start, type "defrag" n the search bar and open Disk Defragmenter.

Change Browsers
Tom's Hardware is a tech site that tests the speed of browsers each year. Their most recent comparison shows Firefox is fastest, then the Chrome browser, Internet Explorer second to last, and then Apple's Safari is slowest.

Even just getting a clean browser — one you haven't fiddled with — can be faster than your previous browser.

Tuesday, October 2, 2012

Types of Skin Cancer

There are five basic types of skin cancer. It is important to watch for signs of these cancers and see a doctor as soon as possible to determine treatment.



Basal Cell Carcinoma

Basal Cell Carcinoma is one of the most common kinds of skin cancer. It looks like a small reddish bump and is commonly found on parts of the body that are exposed to the sun. Basal Cell Carcinoma rarely metastasizes, but it can grow and cause harm to the surrounding bone and tissue. This cancer is slow growing, but should be treated as soon as it is noticed.


Melanoma

Melanoma is a very serious form of skin cancer and, while uncommon, it is the leading cause of all skin cancer deaths. The appearance of a black or brown pigmented spot on the skin should be looked at by a doctor. Melanomas are irregularly colored and asymmetrical in shape.


Kaposi's Sarcoma

A very rare form of skin cancer is Kaposi's Sarcoma. This is caused by the herpes virus and not by sun exposure.


Actinic Keratosis and Squamous Cell Carcinoma

The last two types of skin cancer are related. Actinic Keratosis is a precursor to Squamous Cell Carcinoma. Actinic Keratosis starts as a small red spot that is commonly found on sun-exposed areas of the body. As this precancerous tissue develops, it can thicken and become scaly in appearance. If left untreated, these spots develop into the most common form of skin cancer, Squamous Cell Carcinoma. Squamous Cell Carcinoma can spread and eventually cause death. If treated early, the recovery rate is high.


Most skin cancer is caused by sun exposure. It is important to minimize your exposure to the sun in order to prevent skin cancer from forming and consult a doctor if you suspect any cancer.

Monday, September 17, 2012

Tanzania Students` Center in Cairo



المركز الثقافي لطلبة تنـزانـيا
Tanzania Students` Center in Cairo
For
Teaching English Language, Swahili & Computer Science, Especially for Beginners

المركز الثقافي لطلبة تنـزانـيا


المركز الثقافي لطلبة تنـزانـيا
Tanzania Students` Center in Cairo
For
Teaching English Language, Swahili & Computer Science, Especially for Beginners  

markazitz@gmail.com

Friday, March 9, 2012

Tanzania Students` Center in Cairo

Tanzania Students` Center in Cairo
For Teaching English Language, Swahili & Computer Science, Especially for Beginners.
 T.S.C.C  is a leader in providing top quality English instruction. The intensive English programs that are designed to develop your English skills quickly and prepare you to communicate effectively.

TSCC will give you the skills you need to successfully reach your English goals, whether your goal is to attend an American university, use English for your career, or simply be able to travel and socialize in English. Our programs give you the expert instruction and personal attention you need to succeed!

 TSCC offers one of the smallest class sizes, with the best, most personal attention from our expert faculty instructors. Students are happy with the very friendly.

In these classes students will learn some listening strategies, grammar, pronunciation, writing, reading, vocabulary, and conversation, while also learning basic survival skills for living in the United States. For example, how to order in a restaurant, tipping/gratuities, how to read a bus schedule, telephone conversation tips, and many more important activities which improve practice in ALL areas of English skills. Field trips around town and the university campus are promoted during or outside of class .