Sunday, January 13, 2013

Afrika ya kati ; makubaliano yatiwa saini


Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Francois Bozize amemfuta kazi waziri wake mkuu na kulivunja baraza lake la mawaziri Jumamosi(12.01.2013)akisafisha njia kwa kuteuliwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa.
Serikali  na  waasi  wa  muungano  wa  Seleka , ambao  walisonga mbele  katika  mashambulizi  yao  hadi  karibu  na  mji  mkuu  Bangui mwezi  uliopita, wamekubaliana  kuunda  serikali  ya  mpito mwishoni mwa   mazungumzo  yao  yaliyofanyika  katika  mji  mkuu  wa  Gabon , Libraville  siku  ya  Ijumaa(11.01.2013).
"Kiongozi  wa  nchi, ameondoa matumizi  ya  amri  iliyotolewa  Aprili  22, 2011, inayohusiana  na  kuteuliwa  kwa  serikali," imesema  amri  ya  rais iliyosomwa  katika  televisheni  ya  taifa. Soma Zai didw.de

No comments: